IQNA

Msikiti Mkongwe Zaidi wa Tehran

IQNA - Msikiti wa Jamia wa Tehran, pia unajulikana kama Msikiti wa Atiq, ndio msikiti kongwe zaidi jijini Tehran, na jengo lake la awali lilijengwa zaidi ya miaka elfu moja iliyopita.

Usanifu wa msikiti unaonyesha maendeleo yake ya taratibu katika vipindi tofauti vya kihistoria. Vitu vya kale vilivyopatikana katika msikiti huo, ambao sasa umesajiliwa kama turathi ya kitaifa, ni vya enzi za Al-e Bouyeh, Safavid na Qajar.