Rangi za Msimu wa Vuli katika eneo la Saadabad ya Tehran
IQNA - Eneo la Kitamaduni na Kihistoria cha Saadabad kaskazini mwa Tehran ni bustani kubwa zaidi ya jiji iliyoko chini ya safu ya Milima ya Alborz.
Bustani ya Hekta 110, ambayo inajumuisha idadi ya majumba, majumba ya makumbusho, mitaro ya jadi ya maji safi ambayo ni maarufu kama qanat, na bustani za maua, huwapa wageni mandhari ya kuvutia wakati wa msimu vuli kutokana na kupuputika majani.