IQNA

Kisomo cha Mbinguni: Msikilize Sheikh Ahmed Abulmaati akisoma Surah Al-Nazi'at

IQNA – Ifuatayo ni qiraa ya Sheikh Ahmed Abulmaati akisoma aya za 27-27 za Surah Al-Nazi'at katika Qur'ani Tukufu

 

Mtume Muhammad (SAW) alisema wakati mmoja kwamba kuisikiliza Qur'ani Tukufu humletea mja thawabu za Mwenyezi Mungu, huku kila herufi ikisikika ikistahiki tendo jema kwa msikilizaji, na kumpandisha msikilizaji katika safu ya wale wanaosoma maandiko matukufu na kupaa kuelekea mbinguni. 
Shirika la habari la IQNA limeratibu na kutoa mfululizo unaoitwa "Kisomo cha Mbinguni," wenye kumbukumbu za kuvutia za wasomaji maarufu Qur’ani Tukufu.