IQNA

Kisomo cha Mbinguni: Msikilize Sheikh Mohammad Rafat akisoma aya za Sura Yusuf

IQNA – Hiki kinachofuata ni kisomo cha aya ya 69 ya Surah Yusuf na qari wa Misri Sheikh Mohammad Rafat.

Mtume Muhammad (SAW) alisema wakati mmoja kwamba kuisikiliza Qur'ani Tukufu humletea mja thawabu za Mwenyezi Mungu, huku kila herufi ikisikika ikistahiki tendo jema kwa msikilizaji, na kumpandisha msikilizaji katika safu ya wale wanaosoma maandiko matukufu na kupaa kuelekea mbinguni. 
Shirika la habari la IQNA limeratibu na kutoa mfululizo unaoitwa "Kisomo cha Mbinguni," wenye kumbukumbu za kuvutia za wasomaji maarufu Qur’ani Tukufu.