Sikiliza Qari wa Iran akisoma Aya za Surah Fussilat
IQNA – Qari mashuhuri wa kimataifa kutoka Iran, Ali Ridha Ridhai, hivi karibuni alisoma aya za Qur’ani Tukufu katika hafla ya Qur’ani iliyofanyika katika haram takatifu ya Imam Ridha (AS) mjini Mashhad, kaskazini-mashariki mwa Iran.
Katika hafla hiyo, alisoma aya za 30 hadi 36 za Surah Fussilat, sura ya 41 ya Qur’ani Tukufu. Sikiliza kisomo chake hapa: