Kwa mujibu wa ripoti ya IQNA, Baladi Omar, ambaye ni qari na hafidh maarufu kutoka Ivory Coast, alishiriki katika kampeni ya Qur’ani ya “Fath” kwa usomaji wa aya za mwanzo za surah hiyo tukufu.
Kampeni hii ya Qur’ani iitwayo “Fath” ilizinduliwa na Shirika la Habari la Kimataifa la Qur’ani (IQNA) kufuatia mashambulizi ya utawala wa Kizayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, katika hali ambapo maadui wa Mapinduzi ya Kiislamu wanajaribu kueneza hofu na kukatisha tamaa miongoni mwa wananchi wa Iran kwa njama mbalimbali.
Lengo la kampeni hii ni kuimarisha moyo wa matumaini na imani miongoni mwa Waislamu kupitia ujumbe wa Qur’ani Tukufu, hasa katika nyakati za mitihani na majaribu.
KWA JINA LA MWENYEEZI MUNGU MWINGI WA REHEMA MWENYE KUREHEMU
2. Ili Mwenyezi Mungu akusamehe makosa yako yaliyo tangulia na yajayo, na akutimizie neema zake, na akuongoe katika Njia Iliyo Nyooka,
3. Na Mwenyezi Mungu akunusuru nusura yenye nguvu