Masjid Kabud ambao pia ni maarufu kama Masjid Moẓaffariya ni msikiti muhimu ulioko katika jiji la Tabriz, Iran. Msikiti huu, pamoja na majengo mengine ya umma, ulijengwa mwaka 1465 Miladia kwa amri ya Shah Jahan, mfalme wa Qara Qoyunlu.
Msikiti huu uliharibiwa vibaya katika tetemeko la ardhi la mwaka Miladia, ambapo ni iwān ya kuingilia pekee ndiyo iliyonusurika. Mwaka 1973, Reza Memaran Benam alianza kuukarabati chini ya usimamizi wa Wizara ya Utamaduni ya Iran. Hata hivyo, vigae bado havijakamilika.