Kwa mujibu wa taarifa ya Shirika la Utamaduni na Mahusiano ya Kiislamu (ICRO), masomo hayo ni kuhusu misingi ya sawt, lahn na tajwid katika usomaji Qur’ani. Aidha washiriki wanajifunza kuhusu tafsiri ya aya za Qur’ani Tukufu.
Masomo hayo yanafanyika kwa njia ya intaneti kupitia jukwaa la WhatsApp na waalimu katika kozi hiyo ni Qarii Sayyid Jasim Mousawi na Sayyed Hassan Esmati ambao wanatoa mafunzo kwa lugha Kiarabu na Kifaransa ambazo hutumika Tunisia
Mafunzo hayo ya Qur’ani mwaka huu yamefanyika kwa njia ya intaneti katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani kutokana na vizingiti vilivyowekwa ili kuzuia kuenea ugonjwa wa corona.