iran

IQNA

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeendesha oparesheni kubwa ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya vituo nane vya kijeshi vya Marekani katika kanda hii, likiitaja hatua hiyo kuwa “jibu madhubuti” dhidi ya uchokozi mpya wa Marekani kwenye ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482414   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28

IQNA – Muda wa usajili kwa wanaharakati na watumishi wa Qur’ani wanaotaka kushiriki katika Msafara wa Qur’ani wa Arbaeen wa Iran wa mwaka 2026 umeongezwa hadi Jumanne, tarehe 30 Juni.
Habari ID: 3482413   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28

IQNA-Rais wa Iran ametoa wito wa ushirikiano wa karibu zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisema Iran imenyoosha “mkono wa urafiki” kwa nchi za kanda hii katika harakati za kutafuta mfumo mpya wa usalama.
Habari ID: 3482398   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24

IQNA-Wairani katika mji mkuu Tehran, majiji, miji na vijiji vyote nchini usiku wa kuamkia leo walikusanyika misikitini na katika vituo vya kidini na barabarani katika marasimu ya kuadhimisha Tasu'a, siku ya tisa ya mwezi Muharram, kuelekea kwenye Siku ya Ashura ya kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein (AS), mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW).
Habari ID: 3482397   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24

IQNA – Makao Makuu ya Arbaeen ya Imam Hussein (AS) nchini Irani yametangaza rasmi tarehe za kuanza kwa usajili wa waumini wanaokusudia kushiriki katika matembezi ya Arbaeen ya mwaka huu nchini Iraq.
Habari ID: 3482389   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/22

IQNA-Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
Habari ID: 3482374   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/18

IQNA – Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani imepongezwa na Papa Leo XIV, ambaye ameielezea kuwa hatua muhimu ya kujiepusha na vita.
Habari ID: 3482371   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/17

IQNA-Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3482361   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/15

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482349   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/11

IQNA – Zaidi ya watu 67,000 wamejiandikisha kushiriki katika Mashindano ya 49 ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambapo hatua ya awali inatarajiwa kuanza mwezi ujao.
Habari ID: 3482343   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/09

IQNA – Katika kauli yenye ukali dhidi ya sera za Rais wa Marekani Donald Trump, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran havina uhalali wa maadili.
Habari ID: 3482334   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeshambulia kambi mbili za anga za Marekani huko Kuwait na vituo vilivyobaki vya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani (US Fifth Fleet) huko Bahrain ili kujibu uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani.
Habari ID: 3482327   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06

IQNA – Mstahiki Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amelaani vikali vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran akivitaja kuwa ni mgogoro usio na msingi, na kusisitiza kuwa vita hivyo ni lazima viishe mara moja kwa ajili ya usalama wa raia wa mataifa mengine, na pia kwa manufaa ya Wamarekani wanaopambana na hali ngumu ya maisha nyumbani kwao.
Habari ID: 3482297   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/29

IQNA – Zaidi ya watu 67,000 wamejisajili kwa ajili ya duru ya 49 ya Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Muda wa mwisho wa usajili, ambao ulikuwa umeongezwa mara moja, umefika tamati siku ya Jumatatu.
Habari ID: 3482289   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/27

IQNA-Katika ujumbe wake kwa mnasaba wa kuwadia msimu wa Hijja ya Nabii Ibrahim (as), Ayatullah Seyyed Mojtaba Hosseini Khamenei, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametaja amali na thikri zilizajaa maana za Hijja na kusema ni ishara za kudumu milele kwa wanadamu kwa ajili ya kuwahamasisha waelekee kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu,
Habari ID: 3482288   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26

IQNA – Kwa kuwasili kwa kundi la mwisho la Wairni mjini Madina kwa ajili ya Hija ya mwaka 1447 (2026), mchakato wa kuwasafirisha waumini kuelekea Ardhi ya Wahyi umekamilika. Zaidi ya waumini 30,000 wamesafiri kutoka nchini humo kwenda Ardhi ya Wahyi kupitia safari za ndege 130 kwa ajili ya Ibada ya Hija mwaka huu.
Habari ID: 3482262   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/20

IQNA – Rais wa Iran Masoud Pezeshkian katika ujumbe wake kwa Papa Leo XIV ameshukuru misimamo ya kimaadili ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, akiyataja kuwa ni ukiukaji wa utawala wa sheria na wa maadili ya kibinadamu.
Habari ID: 3482246   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16

Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa
IQNA-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa kimesema kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na “kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu” na kwa hivyo ni “haramu kabisa.”
Habari ID: 3482238   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/14

IQNA – Papa Leo XIV amemtunuku Hujjatul‑Islam Mohammad Hossein Mokhtari, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Vatican, nishani ya juu zaidi ya kidiplomasia ya Vatican.
Habari ID: 3482235   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

IQNA – Mufti Mkuu wa Oman ametoa wito kwa Waislamu kusimama kwa umoja katika kukabiliana na mashambulizi ya utawala wa Kizayuni wa Israel katika ardhi za Kiislamu.
Habari ID: 3482224   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/10