iran

IQNA

IQNA – Mkuu wa Makao Makuu ya Kati ya Arbaeen nchini Iran amesisitiza umuhimu wa matembezi ya kila mwaka ya Arbaeen kama fursa adhimu ya kueneza utamaduni wa Qur’ani.
Habari ID: 3482521   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/21

IQNA – Muungano wa Walimu wa Marekani (American Federation of Teachers - AFT) umeitupia lawama utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kusababisha mgogoro wa walimu katika ardhi za Palestina, huku ukitoa wito wa kukomeshwa kwa uchokozi dhidi ya Lebanon na kuondolewa kwa mzingiro haramu uliowekwa kwenye bandari za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482520   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/21

IQNA – Vituo vyote ya mipakainayoelekea nchini Iraq sasa vinafanya kazi kikamilifu na viko tayari kurahisisha uingiaji na utokaji wa wafanyaziyara wa Arbaeen, amesema afisa mmoja wa Iran.
Habari ID: 3482516   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/20

IQNA-Iran imeonya kwamba italenga kila miundombinu iliyosalia katika eneo hili iwapo miundombinu yake itashambuliwa.
Habari ID: 3482494   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/16

IQNA – Vatikani (Vatican) imekataa jaribio la balozi wa utawala wa Trump katika Vatikan la kuwasilisha ukosoaji wa Papa Leo wa XIV dhidi ya vita vya Marekani dhidi ya Iran kana kwamba ulikuwa uingiliaji wa kisiasa badala ya msimamo wa kidini.
Habari ID: 3482484   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/14

IQNA-Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo asubuhi vimetekeleza operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Qatar, Oman na Bahrain, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi endelevu ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
Habari ID: 3482473   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/12

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeendesha oparesheni kubwa ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya vituo nane vya kijeshi vya Marekani katika kanda hii, likiitaja hatua hiyo kuwa “jibu madhubuti” dhidi ya uchokozi mpya wa Marekani kwenye ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482414   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28

IQNA – Muda wa usajili kwa wanaharakati na watumishi wa Qur’ani wanaotaka kushiriki katika Msafara wa Qur’ani wa Arbaeen wa Iran wa mwaka 2026 umeongezwa hadi Jumanne, tarehe 30 Juni.
Habari ID: 3482413   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28

IQNA-Rais wa Iran ametoa wito wa ushirikiano wa karibu zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisema Iran imenyoosha “mkono wa urafiki” kwa nchi za kanda hii katika harakati za kutafuta mfumo mpya wa usalama.
Habari ID: 3482398   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24

IQNA-Wairani katika mji mkuu Tehran, majiji, miji na vijiji vyote nchini usiku wa kuamkia leo walikusanyika misikitini na katika vituo vya kidini na barabarani katika marasimu ya kuadhimisha Tasu'a, siku ya tisa ya mwezi Muharram, kuelekea kwenye Siku ya Ashura ya kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein (AS), mjukuu wa Mtume Muhammad (SAW).
Habari ID: 3482397   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24

IQNA – Makao Makuu ya Arbaeen ya Imam Hussein (AS) nchini Irani yametangaza rasmi tarehe za kuanza kwa usajili wa waumini wanaokusudia kushiriki katika matembezi ya Arbaeen ya mwaka huu nchini Iraq.
Habari ID: 3482389   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/22

IQNA-Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
Habari ID: 3482374   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/18

IQNA – Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani imepongezwa na Papa Leo XIV, ambaye ameielezea kuwa hatua muhimu ya kujiepusha na vita.
Habari ID: 3482371   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/17

IQNA-Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3482361   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/15

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482349   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/11

IQNA – Zaidi ya watu 67,000 wamejiandikisha kushiriki katika Mashindano ya 49 ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, ambapo hatua ya awali inatarajiwa kuanza mwezi ujao.
Habari ID: 3482343   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/09

IQNA – Katika kauli yenye ukali dhidi ya sera za Rais wa Marekani Donald Trump, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran havina uhalali wa maadili.
Habari ID: 3482334   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07

IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeshambulia kambi mbili za anga za Marekani huko Kuwait na vituo vilivyobaki vya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani (US Fifth Fleet) huko Bahrain ili kujibu uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani.
Habari ID: 3482327   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06

IQNA – Mstahiki Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amelaani vikali vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran akivitaja kuwa ni mgogoro usio na msingi, na kusisitiza kuwa vita hivyo ni lazima viishe mara moja kwa ajili ya usalama wa raia wa mataifa mengine, na pia kwa manufaa ya Wamarekani wanaopambana na hali ngumu ya maisha nyumbani kwao.
Habari ID: 3482297   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/29

IQNA – Zaidi ya watu 67,000 wamejisajili kwa ajili ya duru ya 49 ya Mashindano ya Kitaifa ya Qur’ani Tukufu ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran. Muda wa mwisho wa usajili, ambao ulikuwa umeongezwa mara moja, umefika tamati siku ya Jumatatu.
Habari ID: 3482289   Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/27