Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Baghdad mapema leo umeshambuliwa kwa maroketi ya helikopta za Marekani. Maafisa wa Marekani wamekiri katika mahojiano yao na shirika la habari la Reuters kwamba, shambulizi hilo limefanyika dhidi ya watu wawili wenye mfungamano na Iran.
Vilevile ndege za zisizo na rubani za Marekani usiku wa Jumapili iliyopita zilishambulia vituo vya harakati ya al Hashdul Shaabi katika mji wa al Qaim kwenye eneo lililoko katika mpaka wa Iraq na Syria na kuua wanachama wasiopungua 25 wa harakati hiyo. Wapiganaji wengine 51 wa al Hashdul Shaabi walijeruhiwa.
Baada ya shambulizi hilo maelfu ya Wairaq walifanya maandamano na mgomo mkubwa mbele ya ubalozi wa Marekani mjini Baghdad wakipinga shambulizi la Marekani dhidi ya vituo vya harakati hiyo. Makundi na vyama mbalimbali vya siasa vya Iraq pia vimepinga vikali shambulizi la Marekani dhidi ya al Hashdul Shaabi.