marekani

IQNA

IQNA – Wakazi wa kitongoji kilichopo kusini mwa Kaunti ya St. Louis, jimboni Missouri nchini Marekani, wameamka mwishoni mwa wiki wakikuta mandhari ya kutia hofu, baada ya njia za waenda kwa miguu na baadhi ya barabara kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3482284    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26

IQNA – Mahmoud Khalil, mwanaharakati Mpalestina, amekata rufaa katika Mahakama Kuu ya Marekani ili kuzuia kufukuzwa kwake nchini humo.
Habari ID: 3482279    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/24

IQNA – Ingawa hujuma ya kigaidi dhidi ya Msikiti wa San Diefo ilitokea umbali wa zaidi ya maili 2,000, huzuni na taharuki yake zilihisiwa moja kwa moja kote Marekani hadi kusini-mashariki mwa jimbo la Michigan siku ya Jumatano.
Habari ID: 3482267    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22

IQNA – Watu watatu waliokuwa ndani ya Msikiti wa Kituo cha Kiislamu cha San Diego nchini Marekani wamepoteza maisha kufuatia hujuma ya kigaidi Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa washambuliaji wawili, ambao ni vijana, pia wamefariki dunia, na kufanya jumla ya watu watano kupoteza maisha katika tukio ambalo maafisa wanaliita shambulizi linaloweza kuwa limechochewa na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3482256    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/19

IQNA – Rais wa Iran Masoud Pezeshkian katika ujumbe wake kwa Papa Leo XIV ameshukuru misimamo ya kimaadili ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, akiyataja kuwa ni ukiukaji wa utawala wa sheria na wa maadili ya kibinadamu.
Habari ID: 3482246    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16

Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa
IQNA-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa kimesema kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na “kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu” na kwa hivyo ni “haramu kabisa.”
Habari ID: 3482238    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/14

IQNA – Papa Leo XIV amemtunuku Hujjatul‑Islam Mohammad Hossein Mokhtari, Balozi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Vatican, nishani ya juu zaidi ya kidiplomasia ya Vatican.
Habari ID: 3482235    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

Rais wa Iran katika Mazungumzo ya Simu na Rais wa Ufaransa:
IQNA-Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Masoud Pezeshkian, amemwambia mwenzake wa Ufaransa, Emmanuel Macron, kuwa Tehran iko tayari kuendelea kwa dhati kupitia njia za kidiplomasia ili kukomesha vita, huku ikisisitiza umuhimu wa kulindwa kwa haki za taifa la Iran.
Habari ID: 3482213    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07

IQNA – Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imeitaka serikali ya Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) kusitisha kujipanga upande mmoja na kushirikiana na pande zinazoiwekea uadui Jamhuri ya Kiislamu.
Habari ID: 3482210    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/07

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Qur’ani Tukufu kutoka Iraq amelaani vikali misimamo ya hivi karibuni ya qari wa Kuwait, Mishary Rashid Al Afasi, inayounga mkono dhulma ya Wa marekani na Wazayuni dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482190    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/02

IQNA-Wazazi  Waislamu nchini Marekani sasa wanatilia mkazo zaidi suala la kuhifadhi Qur’an, jambo linalojulikana kama Hifdh.
Habari ID: 3482186    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/01

IQNA-Ayatullah Seyyed Mojtaba Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ametangaza mwanzo wa “sura mpya” kwa Mlango Bahari wa Hormuz, njia ya kimkakati ya baharini.
Habari ID: 3482185    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/01

IQNA – Mtaalamu wa Qur’ani Tukufu kutoka Lebanon amekosoa misimamo ya qari mmoja kutoka Kuwait akisema kuwa haina uhusiano na mafundisho ya Qur’ani.
Habari ID: 3482177    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/29

IQNA – Akikosoa kwa ukali misimamo ya qari wa Kuwait, Mishary Rashid al‑Afasi, katika kuhalalisha mashambulizi ya Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel dhidi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, msomaji wa Qur’ani kutoka Yemen ametoa wito wa kususiwa kwa al‑Afasi.
Habari ID: 3482173    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/28

IQNA – Katika barua mpya aliyoandika kwa Kiongozi wa Kanisa Katoliki Papa Leo wa Kumi na Nne, Mkuu wa Kitengo cha Masomo ya Kiislamu katika Akademia ya Sayansi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ametoa shukrani kwa msimamo wake wa haki katika kukataa mienendo ya ukatili.
Habari ID: 3482172    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/28

IQNA – Visa vya chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia) na mashambulizi dhidi ya Waislamu wa Marekani na taasisi zao vimeongezeka mara kumi na moja (1,000%) katika miezi mitatu ya kwanza ya mwaka 2026, na kufikia kiwango cha juu zaidi katika kipindi cha miezi 15, kwa mujibu wa ripoti mpya ya Kamati ya Masuala ya Umma ya Waislamu (Mpac).
Habari ID: 3482147    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/17

IQNA-Rais wa Iran amesema kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaendelea kusimama upande wa amani, utulivu na mahusiano ya kindugu katika eneo, akibainisha kwamba usalama wa eneo unapaswa kuhakikishwa na mataifa ya eneo hilo yenyewe.
Habari ID: 3482145    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/17

IQNA – Kama ilivyo kwa baadhi ya mataifa mengine katika eneo la Asia Magharibi, wananchi wa Iraq wamejitokeza kusherehekea kile walichokitaja kuwa ushindi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran dhidi ya Marekani na utawala wa Kizayuni.
Habari ID: 3482128    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/08

IQNA-Baraza Kuu la Usalama wa Taifa limetoa taarifa kuhusu ushindi wa kihistoria wa Iran katika vita vya tatu vilivyolazimishwa dhidi yake, pamoja na kukubaliwa kwa masharti ya Iran na upande wa adui.
Habari ID: 3482126    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/08

IQNA-Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limetungua ndege ya pili ya kisasa ya Marekani aina ya F-35 ikiwa katika anga katikati ya Iran kwa kutumia mfumo mpya wa ulinzi wa anga wa Kikosi cha Anga cha jeshi hilo.
Habari ID: 3482114    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/03