Mtazamo
IQNA – Mchambuzi wa kisiasa kutoka Lebanon anaamini kuwa mvutano unaoendelea katika Lango Bahari La Hormuz si mapambano ya kawaida juu ya njia ya majini, bali ni vita vikali vya kuamua hatima na utambulisho wa mfumo wa kiusalama katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482543 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/27
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, ameisifu harakati ya Hizbullah kwa msimamo wake thabiti na usioyumba katika kukabiliana na utawala wa Kizayuni wa Israel na kusema, kuwa uimara wa harakati hiyo ya Lebanon ni ujumbe wenye nguvu wa ukombozi kwa mataifa yaliyodhulumiwa duniani kote.
Habari ID: 3482542 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/27
IQNA – Muungano wa Walimu wa Marekani (American Federation of Teachers - AFT) umeitupia lawama utawala wa Kizayuni wa Israel kwa kusababisha mgogoro wa walimu katika ardhi za Palestina, huku ukitoa wito wa kukomeshwa kwa uchokozi dhidi ya Lebanon na kuondolewa kwa mzingiro haramu uliowekwa kwenye bandari za Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482520 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/21
IQNA – Mfanyakazi mmoja Mwislamu wa vibanda vya biashara amechomwa kisu zaidi ya mara 15 ndani ya kituo cha ununuzi (mall) huko Utah, Marekani, na mtu ambaye baadaye alikiri kwa polisi kuwa alikusudia kumuua “kwa sababu ya dini yake.”
Habari ID: 3482498 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/17
IQNA-Iran imeonya kwamba italenga kila miundombinu iliyosalia katika eneo hili iwapo miundombinu yake itashambuliwa.
Habari ID: 3482494 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/16
IQNA – Vatikani (Vatican) imekataa jaribio la balozi wa utawala wa Trump katika Vatikan la kuwasilisha ukosoaji wa Papa Leo wa XIV dhidi ya vita vya Marekani dhidi ya Iran kana kwamba ulikuwa uingiliaji wa kisiasa badala ya msimamo wa kidini.
Habari ID: 3482484 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/14
IQNA-Vikosi vya Ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran leo asubuhi vimetekeleza operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani nchini Jordan, Kuwait, Qatar, Oman na Bahrain, ikiwa ni hatua ya kujibu mashambulizi endelevu ya Marekani dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
Habari ID: 3482473 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/12
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza rasmi kuwa, katika hatua ya kwanza ya kujibu uchokozi wa Marekani wa usiku wa kuamkia leo, vikosi vya wanamaji na anga vya Jeshi hilo, katika operesheni ya pamoja ya makombora na ndege zisizo na rubani (drones), vimetekeleza kwa mafanikio mashambulizi makali dhidi ya shabaha 85 muhimu vya kijeshi la Marekani na kutungua ndege moja ya kisasa ya kijasusi ya adui aina ya MQ9.
Habari ID: 3482458 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/08
IQNA-Wakati shughuli za mazishi na kuaga mwili wa Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, zikiendelea nchini Iran, Waislamu na wafuasi wake nchini Marekani wameungana kufanya ibada za maombolezo kufuatia kuondoka kwa kiongozi huyo.
Habari ID: 3482449 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/07/06
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeendesha oparesheni kubwa ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya vituo nane vya kijeshi vya Marekani katika kanda hii, likiitaja hatua hiyo kuwa “jibu madhubuti” dhidi ya uchokozi mpya wa Marekani kwenye ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482414 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28
IQNA-Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Mkataba wa Maelewano (MoU) wa kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa matokeo ya shinikizo au kulazimishwa, bali ni zao la ustahimilivu na nguvu ya taifa shupavu la Iran.
Habari ID: 3482399 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA-Rais wa Iran ametoa wito wa ushirikiano wa karibu zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisema Iran imenyoosha “mkono wa urafiki” kwa nchi za kanda hii katika harakati za kutafuta mfumo mpya wa usalama.
Habari ID: 3482398 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA – Mwigizaji maarufu wa Hollywood, Giancarlo Esposito, amethibitisha kuingia kwake katika dini ya Kiislamu baada ya kutamka Shahada, nguzo kuu ya imani ya Kiislamu, na kushiriki katika ibada ya swala msikitini pamoja na wahudumu wenzake wa uzalishaji wa filamu.
Habari ID: 3482393 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/23
IQNA – Rais wa msikiti mmoja mjini Milwaukee, katika jimbo la Wisconsin nchini Marekani, ambaye ameachiliwa huru kutoka kizuizini na Idara ya Uhamiaji (ICE) wiki hii, amesema kuwa amekuwa akilengwa kutokana na msimamo wake thabiti wa kutetea haki za Wapalestina.
Habari ID: 3482381 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/20
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema maafisa wa Iran wamefanya juhudi kubwa kwa nia njema na kwa kujali maslahi ya taifa ili kufikia hati ya makubaliano (MoU) na Marekani, huku rais wa Marekani akitumia mbinu mbalimbali kutokana na hali ya kukata tamaa.
Habari ID: 3482379 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/19
IQNA-Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
Habari ID: 3482374 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/18
IQNA – Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani imepongezwa na Papa Leo XIV, ambaye ameielezea kuwa hatua muhimu ya kujiepusha na vita.
Habari ID: 3482371 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/17
IQNA-Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3482361 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/15
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482349 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/11
IQNA – Meya Mwislamu wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, siku ya Jumatano alipinga vikali mipango ya utawala wa Trump ya kuongeza uwepo wa maafisa wa Idara ya Uhamiaji, kwa kifupi ICE, jijini humo wakati wa mashindano ya Kombe la Dunia.
Habari ID: 3482345 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/10