IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeendesha oparesheni kubwa ya makombora na ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya vituo nane vya kijeshi vya Marekani katika kanda hii, likiitaja hatua hiyo kuwa “jibu madhubuti” dhidi ya uchokozi mpya wa Marekani kwenye ardhi ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Habari ID: 3482414 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/28
IQNA-Spika wa Bunge la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Mkataba wa Maelewano (MoU) wa kumaliza vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran haukuwa matokeo ya shinikizo au kulazimishwa, bali ni zao la ustahimilivu na nguvu ya taifa shupavu la Iran.
Habari ID: 3482399 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA-Rais wa Iran ametoa wito wa ushirikiano wa karibu zaidi miongoni mwa nchi za Kiislamu, akisema Iran imenyoosha “mkono wa urafiki” kwa nchi za kanda hii katika harakati za kutafuta mfumo mpya wa usalama.
Habari ID: 3482398 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/24
IQNA – Mwigizaji maarufu wa Hollywood, Giancarlo Esposito, amethibitisha kuingia kwake katika dini ya Kiislamu baada ya kutamka Shahada, nguzo kuu ya imani ya Kiislamu, na kushiriki katika ibada ya swala msikitini pamoja na wahudumu wenzake wa uzalishaji wa filamu.
Habari ID: 3482393 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/23
IQNA – Rais wa msikiti mmoja mjini Milwaukee, katika jimbo la Wisconsin nchini Marekani, ambaye ameachiliwa huru kutoka kizuizini na Idara ya Uhamiaji (ICE) wiki hii, amesema kuwa amekuwa akilengwa kutokana na msimamo wake thabiti wa kutetea haki za Wapalestina.
Habari ID: 3482381 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/20
IQNA – Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema maafisa wa Iran wamefanya juhudi kubwa kwa nia njema na kwa kujali maslahi ya taifa ili kufikia hati ya makubaliano (MoU) na Marekani, huku rais wa Marekani akitumia mbinu mbalimbali kutokana na hali ya kukata tamaa.
Habari ID: 3482379 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/19
IQNA-Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Marekani sasa imetiwa saini rasmi na marais wa nchi hizo mbili baada ya maandishi yake kukamilishwa, na hivyo makubaliano hayo kuanza kutekelezwa. Hayo yametangazwa na msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran Jumatano usiku.
Habari ID: 3482374 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/18
IQNA – Hati ya makubaliano (MoU) kati ya Iran na Marekani imepongezwa na Papa Leo XIV, ambaye ameielezea kuwa hatua muhimu ya kujiepusha na vita.
Habari ID: 3482371 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/17
IQNA-Sekretarieti ya Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran (SNSC) imethibitisha kuwa Iran na Marekani zimekamilisha maandishi ya hati ya makubaliano (MoU) yanayolenga kumaliza vita, kusimamisha mara moja na kwa kudumu operesheni zote za kijeshi katika nyanja zote, ikiwemo Lebanon, na pia kuondoa mzingiro wa baharini uliowekwa na Marekani dhidi ya Iran.
Habari ID: 3482361 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/15
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) likishirikiana na Jeshi la Kitaifa la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran (Artesh), limetangaza mfululizo wa operesheni za kijeshi za kulipiza kisasi zilizoratibiwa vyema dhidi ya kambi za kijeshi za Marekani katika eneo la Asia Magharibi.
Habari ID: 3482349 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/11
IQNA – Meya Mwislamu wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, siku ya Jumatano alipinga vikali mipango ya utawala wa Trump ya kuongeza uwepo wa maafisa wa Idara ya Uhamiaji, kwa kifupi ICE, jijini humo wakati wa mashindano ya Kombe la Dunia.
Habari ID: 3482345 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/10
IQNA – Katika kauli yenye ukali dhidi ya sera za Rais wa Marekani Donald Trump, Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani amesema kwamba vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran havina uhalali wa maadili.
Habari ID: 3482334 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/07
IQNA-Jeshi la Iran la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limeshambulia kambi mbili za anga za Marekani huko Kuwait na vituo vilivyobaki vya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani (US Fifth Fleet) huko Bahrain ili kujibu uchokozi wa hivi karibuni wa Marekani.
Habari ID: 3482327 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/06
IQNA – Mstahiki Meya wa Jiji la New York, Zohran Mamdani, amelaani vikali vita vya Marekani na Israel dhidi ya Iran akivitaja kuwa ni mgogoro usio na msingi, na kusisitiza kuwa vita hivyo ni lazima viishe mara moja kwa ajili ya usalama wa raia wa mataifa mengine, na pia kwa manufaa ya Wamarekani wanaopambana na hali ngumu ya maisha nyumbani kwao.
Habari ID: 3482297 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/29
IQNA – Wakazi wa kitongoji kilichopo kusini mwa Kaunti ya St. Louis, jimboni Missouri nchini Marekani, wameamka mwishoni mwa wiki wakikuta mandhari ya kutia hofu, baada ya njia za waenda kwa miguu na baadhi ya barabara kuchafuliwa kwa maandishi ya chuki dhidi ya Waislamu.
Habari ID: 3482284 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/26
IQNA – Mahmoud Khalil, mwanaharakati Mpalestina, amekata rufaa katika Mahakama Kuu ya Marekani ili kuzuia kufukuzwa kwake nchini humo.
Habari ID: 3482279 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/24
IQNA – Ingawa hujuma ya kigaidi dhidi ya Msikiti wa San Diefo ilitokea umbali wa zaidi ya maili 2,000, huzuni na taharuki yake zilihisiwa moja kwa moja kote Marekani hadi kusini-mashariki mwa jimbo la Michigan siku ya Jumatano.
Habari ID: 3482267 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/22
IQNA – Watu watatu waliokuwa ndani ya Msikiti wa Kituo cha Kiislamu cha San Diego nchini Marekani wamepoteza maisha kufuatia hujuma ya kigaidi Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa washambuliaji wawili, ambao ni vijana, pia wamefariki dunia, na kufanya jumla ya watu watano kupoteza maisha katika tukio ambalo maafisa wanaliita shambulizi linaloweza kuwa limechochewa na chuki dhidi ya Uislamu.
Habari ID: 3482256 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/19
IQNA – Rais wa Iran Masoud Pezeshkian katika ujumbe wake kwa Papa Leo XIV ameshukuru misimamo ya kimaadili ya kiongozi huyo wa Kanisa Katoliki kuhusu mashambulizi ya hivi karibuni ya Marekani na Israel dhidi ya Iran, akiyataja kuwa ni ukiukaji wa utawala wa sheria na wa maadili ya kibinadamu.
Habari ID: 3482246 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/16
Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa
IQNA-Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Al-Mustafa kimesema kuwa ushiriki, uwezeshaji na ushirikiano wa Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE) katika vita vya hivi karibuni vya uchokozi vilivyoanzishwa na Marekani pamoja na utawala wa Israel dhidi ya Iran ni sawa na “kusaidia kambi ya ukafiri dhidi ya ndugu Waislamu” na kwa hivyo ni “haramu kabisa.”
Habari ID: 3482238 Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/14