iqna

IQNA

IQNA – Wabunge wote Waislamu wa Bunge la Marekani wametoa taarifa ya pamoja kulaani mashambulizi ya chuki dhidi ya Uislamu yaliyomlenga Zohran Mamdani, mgombea wa Umeya wa Jiji la New York, ambayo yametokea kutoka kwa wanasiasa wa chama tawala cha Warepublican na hata baadhi ya Wademocrat.
Habari ID: 3480866    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/28

IQNA – Baraza la Mahusiano ya Kiislamu na Marekani (CAIR) limemtaja mbunge katika Bunge la Marekani Randy Fine (R-FL) kuwa “mwenye msimamo mkali wa chuki dhidi ya Waislamu”, likimjumuisha katika orodha yake ya watu wenye chuki dhidi ya Uislamu (Islamophobia), kutokana na kile ilichokiita rekodi ya muda mrefu ya matamshi ya uchochezi dhidi ya Waislamu na Wapalestina.
Habari ID: 3480821    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/11

IQNA – Malalamiko ya ukiukaji wa haki za kiraia yamewasilishwa kwa Idara ya Haki za Kiraia ya Jimbo la Michigan nchini Marekani dhidi ya tawi la Domino’s Pizza lililoko Waterford, kufuatia ripoti ya ubaguzi wa kidini na uharibifu wa chakula uliowalenga wanawake wawili Waislamu na watoto wao.
Habari ID: 3480803    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/07

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema urutubishaji wa urani ndio ufunguo wa suala la nyuklia la Iran, akipuuzilia mbali pendekezo la Marekani kwa Tehran la kusimamisha kikamilifu urutubishaji wa madini hayo (ya urani).
Habari ID: 3480785    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/06/04

IQNA-Kwa mujibu wa taarifa, mnamo Ijumaa, Juni 6, Waislamu wa Marekani wanapanga kuadhimisha mwanzo wa sikukuu hii inayohitimisha ibada ya Hija kwa kuswali pamoja na kusherehekea katika maeneo mbalimbali nchini humo. 
Habari ID: 3480761    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/30

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amekosoa matamshi ya hivi karibuni ya Rais Donald Trump wa Marekani na kuyataja kuwa ni "fedheha" kwa taifa la Marekani.
Habari ID: 3480694    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/17

IQNA – Waislamu wanaosimamia mradi wa ujenzi wa mtaa wao mpya huko Texas, Marekani wamesema uchunguzi wa serikali na shirikisho una dosari.
Habari ID: 3480665    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/10

IQNA – Mohsen Mahdawi, mwanafunzi wa Kipalestina katika Chuo Kikuu cha Columbia nchini Marekani aliyekamatwa kwa kushiriki maandamano kupinga vita vya Israel dhidi ya Gaza, ameachiwa huru kutoka kizuizini.
Habari ID: 3480623    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/05/02

IQNA – M marekani mwenye asili ya Kiarabu amefungua kesi ya ubaguzi dhidi ya Shirika la Big Jay’s Auto Sales huko Shelby Township, Michigan, Marekani akidai kwamba mfanyakazi wa shirika hilo  alitoa matamshi ya udhalilishaji kuhusu imani yake ya Uislamu wakati wa mazungumzo ya uuzaji wa gari. 
Habari ID: 3480592    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/25

IQNA – Wanafunzi watatu Waislamu wa chuo kikuu huko Georgia nchini Marekani wametozwa faini ya kifedha baada ya kudhalilishwa walipokuwa wakiswali katika eneo la maegesho ya umma.
Habari ID: 3480548    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/16

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Seyyed Ali Khamenei amesema mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja kati ya Iran na Marekani katika mji mkuu wa Oman, Muscat, yamefanyika vizuri katika hatua za awali, lakini ameongeza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ina shaka kubwa kuhusu upande wa pili.
Habari ID: 3480545    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/04/15

IQNA – Mashindano ya Qur'ani kwa watoto yamefanyika Charlotte, jimbo la North Carolina, Marekani katika Mwezi Mtukufu  Ramadhani. 
Habari ID: 3480440    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/26

IQNA-Vikosi vya Jeshi la Yemeni vimetangaza shambulio jingine dhidi ya vikosi vya Marekani katika eneo la Bahari ya Shamu, vikitumia makombora na ndege zisizo na rubani ili kuzuia shambulio tarajiwa la Marekani dhidi ya nchi hiyo ya Kiarabu.
Habari ID: 3480393    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/18

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Sayyid Ali Khamenei amesema, ombi la Rais Donald Trump wa Marekani kwamba anataka kufanya mazungumzo na Iran si lolote bali ni jaribio la "kuhadaa maoni ya umma duniani" na kutaka kuonyesha kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ni upande ambao hauko tayari kutoa fursa nyingine kwa diplomasia.
Habari ID: 3480365    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/13

IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Seyyid Ali Khamenei, amesema kuwa sisitizo la baadhi ya madola ya kibabe juu ya kuandaa mazungumzo na Iran hakulengi kutatua matatizo.
Habari ID: 3480330    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/03/09

IQNA – Wanafunzi Waislamu katika shule moja ya California ambao wanafunga wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani watapewa ‘chakula cha kubeba’ na shule hiyo.
Habari ID: 3480251    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/22

IQNA – Wazazi na walimu nchini Marekani wametakiwa kuhudhuria webinari (warsha za mtandaoni) mbili zijazo zinazolenga kuunga mkono wanafunzi Waislamu wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3480210    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/02/13

IQNA – Kufuatia moto mbaya huko Los Angeles, California nchini Marekani ambao umeuteketeza Msikiti wa At-Taqwa, jamii ya Waislamu imekusanya zaidi ya dola 745,000 kwa ajili ya kujenga upya msikiti huo.
Habari ID: 3480067    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/17

Waislamu Marekani
IQNA – Mji wa Michiganu Januari kuwa "Mwezi wa Urithi wa Waislamu wa Marekani," ili kutambua michango muhimu ya Waislamu wa Marekani katika utamaduni, uchumi, na jamii katika jimbo hilo.
Habari ID: 3480036    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/11

Diplomasia ya Muqawama
IQNA-Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Ali Khamenei, amesisitizia wajibu wa kupambana na uvamizi wa Marekani nchini Iraq sambamba na kuimarisha kikosi cha kujitolea cha wananchi wa Iraq maarufu kwa jina la al-Hashd al-Shaabi.
Habari ID: 3480022    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/01/09