IQNA

Kijana Mmisri akisoma Sura Maryam kwa sauti yenye mvuto + Video

Qarii kijana Mmisri Hani Al Azouni anasema Sura Maryam kwa sauti yenye mvuto na mtindo wa aina yake. Katika kilipu hii anasoma aya za 1-8 za Sura Maryam
  1. Kaf Ha Ya A'yn S'ad. 
  2. Huu ni Ukumbusho wa rehema ya Mola wako Mlezi kwa mja wake, Zakariya. 
  3. Alipo mwita Mola wake Mlezi kwa siri. 
  4. Akasema: Mola wangu Mlezi! Mafupa yangu yamedhoofika, na kichwa kinameremeta kwa mvi; wala, Mola wangu Mlezi, sikuwa mwenye bahati mbaya kwa kukuomba Wewe. 
  5. Na hakika mimi nawakhofia jamaa zangu baada yangu. Na mke wangu ni tasa. Basi nipe mrithi kutoka kwako. 
  6. Atakaye nirithi mimi na awarithi ukoo wa Yaaqub. Ewe Mola wangu Mlezi! Na umjaalie awe mwenye kuridhisha. 
  7. (Akaambiwa): Ewe Zakariya! Hakika Sisi tunakubashiria mwana; jina lake ni Yahya. Hatujapata kumpa jina hilo yeyote kabla yake. 
  8. Akasema: Ewe Mola wangu Mlezi! Vipi nitakuwa na mwana na hali mke wangu ni tasa, na mimi nimesha fikia ukongwe katika uzee? 
Kishikizo: misri ، qurani tukufu ، azouni