misri

IQNA

IQNA – Mashindano ya kimataifa ya Qur’ani ya Misri ya mwaka huu yatafanyika kwa kumbukumbu ya qari mashuhuri marehemu Sheikh Abdel Fattah Shaasha’i.
Habari ID: 3482326    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/05

IQNA – Idhaa ya Qur’ani Tukufu ya Misri, yenye makao yake Cairo, imeanza kurusha hewani usomaji wa Qur’ani kwa mtindo wa tarteel wa miaka ya 1960 wa qari mashuhuri Sheikh Mohamed Siddiq El‑Minshawi.
Habari ID: 3482318    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/03

IQNA – Chuo cha Kimataifa cha Al-Azhar nchini Misri kiliandaa programu ya ziara ya maimamu, wahubiri na walinganiaji wageni kutembelea vivutio vya kihistoria vya Kiislamu na Kikristo katika eneo la Fustat.
Habari ID: 3482315    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/06/02

IQNA – Wengi wanaamini kuwa kurekodiwa kwa Surat Yusuf kulikuwa mgeuko wa kweli katika maisha ya Sheikh al-Sayyid Saeed, na mafanikio hayo makubwa yakamfanya ajipatie umaarufu na hatimaye kunyakua lakabu inayostahiki ya “Sultan al-Qurra” (Mfalme wa Wasomaji Qur’ani).
Habari ID: 3482308    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/31

IQNA – Kijana mdogo kutoka nchini Misri amewastaajabisha waandaaji wa programu ya Siku ya Qur’ani nchini Oman, baada ya kufanikiwa kusoma Qur'ani Tukufu nzima kwa kichwa (hifdhu) ndani ya muda wa saa nane pekee, akionyesha ustadi wa hali ya juu na weledi wa kustaajabisha.
Habari ID: 3482280    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/25

IQNA – Ofisi ya Amal ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu imezinduliwa rasmi katika hafla maalumu iliyoandaliwa katika Mkoa wa Sinai, nchini Misri.
Habari ID: 3482239    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/15

CAIRO – Vikosi vya usalama jijini Cairo, Misri, vimefunga duka la vitabu lililokuwa linafanya kazi bila kibali katika eneo la Darb al‑Ahmar baada ya kubainika kuwa lilikuwa likisambaza na kuuza nakala za Qur’ani Tukufu (Misahafu) bila kupata vibali vinavyotakiwa kisheria.
Habari ID: 3482234    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

IQNA – Wizara ya Awqaf ya Misri imetangaza uungaji mkono wake kamili kwa vituo vya kuhifadhi Qur’ani Tukufu pamoja na kuendeleza programu zake za kielimu na kimaadili.
Habari ID: 3482225    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/11

IQNA – Sheikh Muhammad Mahmoud Tablawi, mmoja wa maqari mashuhuri na wenye taswira ya kipekee nchini Misri, alifariki dunia miaka sita iliyopita baada ya kutumikia Qur'ani Tukufu kwa zaidi ya miaka sitini.
Habari ID: 3482220    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/09

IQNA – Sheikh Muhammad Abdulaziz Hissan, qari mashuhuri wa Misri aliyekuwa na ulemavu wa macho, alikuwa na shule ya kipekee ya sauti na maqam, na aliacha nyuma mamia ya kanda za usomaji wa Qur’ani Tukufu ambazo bado zinatangazwa na vyombo vya habari vya Misri na nje ya Misri.
Habari ID: 3482202    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/05

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Ibtihal kutoka Misri na jaji wa mashindano ya Qur’ani ametangaza kuwa atatayarisha kasida yenye maudhui ya Qur’ani ili kukabiliana na mashambulizi ya yaliyofanywa na qari mmoja kutoka Kuwait dhidi ya Iran na mhimili wa muqawama.
Habari ID: 3482162    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/25

IQNA – Makumbusho ya Kitaifa ya Ustaarabu wa Misri yamefanikiwa kurekebisha na kulinda baadhi ya nakala adimu za Qur’ani Tukufu zilizoandikwa kwa mkono.
Habari ID: 3482127    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/08

IQNA – Idara ya Shule ya Kituo cha Kiislamu cha Al‑Azhar nchini Misri imebuni aplikesheni mpya ya kielimu iitwayo “Usomaji wa Qur’ani kwa Njia ya Kielektroniki” kwa ajili ya wanafunzi wa shule.
Habari ID: 3482116    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/04

IQNA – Mitihani ya hatua ya awali ya Mashindano ya 33 ya Kimataifa la Misri la Kuhifadhi na Kufahamu Qur’ani Tukufu yanatarajiwa kuanza siku ya Jumapili, tarehe 5 Aprili.
Habari ID: 3482101    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/29

IQNA — Wizara ya Awqaf ya Misri imetangaza kuwatuma wasomaji wa Qur’ani na maimamu katika nchi 22 wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3481953    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/18

IQNA – Siku ya Jumamosi, tarehe 14 Februari, iliadhimishwa kumbukumbu ya kifo cha qari na msomaji mashuhuri wa ibtihal wa Misri, marehemu Sheikh Sayyid Mohamed al‑Naqshbandi, mmoja wa nguzo kuu za ibada na hisia za Mwezi Mtukufu Ramadhani nchini Misri na ulimwengu wa Kiarabu.
Habari ID: 3481940    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/15

IQNA – Ingawa kipindi cha vipaji vya Qur’ani cha Misri “Dawlat El‑Tilawah" bado hakijafikia hatua ya fainali, Maqari au wasomaji wawili waliobainika kwa umahiri wao katika kipindi hicho walitunukiwa zawadi katika hafla rasmi iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Cairo.
Habari ID: 3481917    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/11

IQNA – Omar Ali Awad ametangazwa na kutunukiwa tuzo ya “Tawi la Dhahabu” katika shindano la vipaji vya Qur’ani lijulikanalo kama “Dawlet El Telawa (Hali ya Usomaji)” nchini Misri.
Habari ID: 3481903    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08

IQNA – Toleo la 9 la Mashindano ya Kimataifa ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu na Ibtihal ya Port Said lilianza rasmi Ijumaa katika mji wa bandari wa Port Said, Misri.
Habari ID: 3481875    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/31

IQNA – Msimamizi mkuu wa mashindano ya vipaji vya Qur’ani nchini Misri, maarufu kwa jina “Dawlat al-Tilawa”, ametangaza kuwa msimu mpya wa kipindi hicho kitaanza rasmi Novemba 2026.
Habari ID: 3481784    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/08