misri

IQNA

IQNA – Ofisi ya Amal ya kuhifadhi Qur’ani Tukufu imezinduliwa rasmi katika hafla maalumu iliyoandaliwa katika Mkoa wa Sinai, nchini Misri.
Habari ID: 3482239    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/15

CAIRO – Vikosi vya usalama jijini Cairo, Misri, vimefunga duka la vitabu lililokuwa linafanya kazi bila kibali katika eneo la Darb al‑Ahmar baada ya kubainika kuwa lilikuwa likisambaza na kuuza nakala za Qur’ani Tukufu (Misahafu) bila kupata vibali vinavyotakiwa kisheria.
Habari ID: 3482234    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/13

IQNA – Wizara ya Awqaf ya Misri imetangaza uungaji mkono wake kamili kwa vituo vya kuhifadhi Qur’ani Tukufu pamoja na kuendeleza programu zake za kielimu na kimaadili.
Habari ID: 3482225    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/11

IQNA – Sheikh Muhammad Mahmoud Tablawi, mmoja wa maqari mashuhuri na wenye taswira ya kipekee nchini Misri, alifariki dunia miaka sita iliyopita baada ya kutumikia Qur'ani Tukufu kwa zaidi ya miaka sitini.
Habari ID: 3482220    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/09

IQNA – Sheikh Muhammad Abdulaziz Hissan, qari mashuhuri wa Misri aliyekuwa na ulemavu wa macho, alikuwa na shule ya kipekee ya sauti na maqam, na aliacha nyuma mamia ya kanda za usomaji wa Qur’ani Tukufu ambazo bado zinatangazwa na vyombo vya habari vya Misri na nje ya Misri.
Habari ID: 3482202    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/05/05

IQNA – Msomaji mashuhuri wa Ibtihal kutoka Misri na jaji wa mashindano ya Qur’ani ametangaza kuwa atatayarisha kasida yenye maudhui ya Qur’ani ili kukabiliana na mashambulizi ya yaliyofanywa na qari mmoja kutoka Kuwait dhidi ya Iran na mhimili wa muqawama.
Habari ID: 3482162    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/25

IQNA – Makumbusho ya Kitaifa ya Ustaarabu wa Misri yamefanikiwa kurekebisha na kulinda baadhi ya nakala adimu za Qur’ani Tukufu zilizoandikwa kwa mkono.
Habari ID: 3482127    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/08

IQNA – Idara ya Shule ya Kituo cha Kiislamu cha Al‑Azhar nchini Misri imebuni aplikesheni mpya ya kielimu iitwayo “Usomaji wa Qur’ani kwa Njia ya Kielektroniki” kwa ajili ya wanafunzi wa shule.
Habari ID: 3482116    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/04/04

IQNA – Mitihani ya hatua ya awali ya Mashindano ya 33 ya Kimataifa la Misri la Kuhifadhi na Kufahamu Qur’ani Tukufu yanatarajiwa kuanza siku ya Jumapili, tarehe 5 Aprili.
Habari ID: 3482101    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/03/29

IQNA — Wizara ya Awqaf ya Misri imetangaza kuwatuma wasomaji wa Qur’ani na maimamu katika nchi 22 wakati wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani.
Habari ID: 3481953    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/18

IQNA – Siku ya Jumamosi, tarehe 14 Februari, iliadhimishwa kumbukumbu ya kifo cha qari na msomaji mashuhuri wa ibtihal wa Misri, marehemu Sheikh Sayyid Mohamed al‑Naqshbandi, mmoja wa nguzo kuu za ibada na hisia za Mwezi Mtukufu Ramadhani nchini Misri na ulimwengu wa Kiarabu.
Habari ID: 3481940    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/15

IQNA – Ingawa kipindi cha vipaji vya Qur’ani cha Misri “Dawlat El‑Tilawah" bado hakijafikia hatua ya fainali, Maqari au wasomaji wawili waliobainika kwa umahiri wao katika kipindi hicho walitunukiwa zawadi katika hafla rasmi iliyofanyika katika Chuo Kikuu cha Cairo.
Habari ID: 3481917    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/11

IQNA – Omar Ali Awad ametangazwa na kutunukiwa tuzo ya “Tawi la Dhahabu” katika shindano la vipaji vya Qur’ani lijulikanalo kama “Dawlet El Telawa (Hali ya Usomaji)” nchini Misri.
Habari ID: 3481903    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/02/08

IQNA – Toleo la 9 la Mashindano ya Kimataifa ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu na Ibtihal ya Port Said lilianza rasmi Ijumaa katika mji wa bandari wa Port Said, Misri.
Habari ID: 3481875    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/31

IQNA – Msimamizi mkuu wa mashindano ya vipaji vya Qur’ani nchini Misri, maarufu kwa jina “Dawlat al-Tilawa”, ametangaza kuwa msimu mpya wa kipindi hicho kitaanza rasmi Novemba 2026.
Habari ID: 3481784    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/08

IQNA – Kipindi cha 12 cha mashindano ya Qur'ani Tukufu ya Dawlat al-Tilawa nchini Misri kiligeuka safari ya kiroho na kihisia, ambapo simulizi binafsi ziliungana na sauti za mbinguni, zikazalisha athari ya kina iliyogusa nyoyo za kila msikilizaji.
Habari ID: 3481773    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/06

IQNA – Sheikh Ahmed Ahmed Nuaina, qari mashuhuri wa Misri, amechapisha kwenye ukurasa wake rasmi wa Facebook video inayoonyesha mwanamke Mmarekani akisilimu katika moja ya misikiti nchini Marekani.
Habari ID: 3481769    Tarehe ya kuchapishwa : 2026/01/05

IQNA – Kipindi cha 13 cha shindano la vipaji vya Qur’ani Tukufu nchini Misri maarufu Dawlat al-Tilawa kilirushwa hewani wiki hii, kikiashiria kuanza kwa hatua ya mwisho ya mashindano.
Habari ID: 3481730    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/28

IQNA – Wachezaji wa timu ya taifa ya kandanda ya Misri wamesoma aya za Qur’ani Tukufu kwa sauti ya pamoja kabla ya mechi dhidi ya Zimbabwe katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON).
Habari ID: 3481714    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/25

IQNA-Mashindano ya kuhifadhi na kusoma Qur’ani yatafanyika katika jimbo la Menoufia, Misri, kwa kumbukumbu ya dada watatu wadogo wa Kimasri waliopoteza maisha katika ajali. Mashindano haya yamepangwa kufanyika katika mwezi mtukufu wa Ramadhani (Februari–Machi, 2026).
Habari ID: 3481711    Tarehe ya kuchapishwa : 2025/12/24