Mkutano huo unasimamiwa na Kituo cha Sayansi na Teknolojia cha Sultan bin Abdulaziz kikishirikiana na Jumuiya ya Kimataifa ya Muujiza wa Kielimu wa Qur’ani na Suna za Mtume Mtukufu.
Mkutano huo utahudhuriwa na watafiti wa masuala ya Qur’ani kutoka nchi kadhaa za Kiislamu ikiwemo Yemen, Oman, Imarati na Saudi Arabia yenyewe.
Makala mbalimbali kuhusu historia na sheria za muujiza wa kielimu wa Qur’ani Tukufu zitawasilishwa katika mkutano huo. 335751