IQNA

Msafara wa Meli wa misaada ya Gaza wafika pwani ya Ugiriki

18:21 - April 29, 2026
Habari ID: 3482179
IQNA – Msafara wa meli unaojulikana kama Global Sumud Flotilla, unaolenga kuvunja mzingiro uliowekwa na utawala katili wa Israeli dhidi ya Wapalestina katika Ukanda wa Gaza, umefika katika maji ya kimataifa karibu na pwani ya Ugiriki.

Kwa mujibu wa Kituo cha Habari cha Palestina, msafara huo unapangiwa kukutana na kundi jingine la meli na boti zilizoondoka katika bandari za Uturuki na Ugiriki ili kuunganisha msafara huo kabla ya kuelekea katika kituo chake cha mwisho.

Wasemaji wa msafara huo walisema kuwa meli zinaendelea na safari yao kulingana na ratiba ya “Spring 2026 Mission”, licha ya kuwepo kwa shinikizo kubwa la kisiasa na kisheria kutoka kwa baadhi ya pande za kimataifa zinazojaribu kuzuia safari hiyo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo, meli za msafara huo ambazo zimebeba wanaharakati kutoka nchi 39 zinaendelea na safari yao, na iwapo hazitazuiliwa baharini, zinatarajiwa kufika katika maji ya Palestina katika siku zijazo.

Mwezi Septemba uliopita, msafara huo uliondoka kutoka Hispania, na hatimaye ulijumuisha boti 43 pamoja na watu 462.

Kabla haujafika Gaza, vikosi katili vya vya Israel vilivamia meli hizo na kuwakamata washiriki waliokuwamo, akiwemo mwanaharakati wa mazingira kutoka Sweden, Greta Thunberg.

3497278

Habari zinazohusiana
captcha