Kituo cha habari cha Thenews kimeripoti kuwa Hamid Said ameliambia bunge la nchi hiyo kwamba tokea sasa serikali itasimamia kwamakini viwango na ubora wa karatasi zinazotumiwa kuchapishia Qur'ani na kwamba wachapishaji wanaotumia karatasi zenye viwango vya chini watachukuliwa hatua za kisheria.
Waziri wa Masuala ya Kidini wa Pakistan amesema: Kwa sasa watu wanaochapisha Qur'ani kwa karatasi zisizokuwa na ubora unaohitajika wanapigwa faini ya rupia elfu tano na kifungo cha jela miaka mitatu na kwamba faini hiyo itaongezwa na kuwa rupia elfu 50. 349623