IQNA

Maariv: Kuchoma Qur'ani katika vita vya Gaza ni kuporomoka kimaadili kwa Israel

12:49 - January 22, 2009
Habari ID: 1734381
Gazeti la Maariv la Israel limeandika kuwa kitendo cha askari wa utawala huo cha kushambulia miskiti na kuchoma moto makala za Qur'ani ni kilele cha kuporomoka kiimadili utawala wa Israel.
Katika makala yake iliyopewa anwani ya "Kushindwa Kimaadili", gazeti hilo limeandika kuwa: Kuharibu misikiti na vituo vya Qur'ani huko Gaza na kuchoma moto kitabu kitukufu cha Waislamu katika kipindi chote cha vita ni kitendo cha kinyama na kisichokuwa cha kimaadili kilichofanywa na askari wa Israel katika vita vya siku 22.
Gazeti hilo la Israel limeashiria kwamba nusu ya waliouawa katika mashambulizi ya Gaza walikuwa wanawake na watoto wadogo na kuhoji kwamba je, lengo la mashambulizi ya Israel katika Ukanda wa Gaza lilikuwa ni kuangamiza harakati ya Hamas au kuvunjia heshima itikadi za Waislamu na kuwaua kwa umati watu wasiokuwa na hatia?
Mwishoni mwa makala hiyo, gazeti la Maariv la Israel limeandika: Kuna ushahidi madhibuti unaothibitisha kwamba jeshi la Israel lilikuwa likishambulia kwa makusudi makazi ya raia, shule na misikiti ya Gaza na kwamba taarifa ya jana ya jeshi la Israel lililokiri kwamba limetumia fosforasi nyeupe na mabomu ya joto katika vita vya Gaza imezitia wasiwai mkubwa jumuiya za kimataifa juu ya utumiaji wa silaha zilizopigwa marufuku. 352246
captcha