IQNA

Mashindano ya kitaifa ya maana ya Qur'ani ya Taasisi ya Wakfu kufanyika Iran

11:57 - January 28, 2009
Habari ID: 1736925
Msimamizi wa Idara ya Masomo na Mashindano ya Taasisi ya Wakfu na Masuala ya Kheri ya Iran amesema kuwa mashindano ya kitaifa ya kufafanua maana ya Qur'ani Tukufu yatafanyika katika mikoa yote nchini humo tarehe 5 Februari sambamba na sherere za kuadhimisha miaka 30 ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
Hayo yamesema na Hujjatul Islam wal Muslimeen Sayyid Muhammad Kadhim Musawi, mkuu wa idara iliyotajwa. Amesema, washindi watatno wa kike na watano wa kiume katika kila mkoa watachaguliwa na kisha kushiriki katika mashindano ya kitaifa ya mafhumu na maana ya Qur'ani Tukufu.
Kadhim Musawi amesema, tayari maswali yatakayoulizwa katika mashindano hayo yamekwishatayarishwa na kwamba yatatumwa hivi karibuni katika idara kuu za taasisi hiyo mikoani. 353775
captcha