IQNA

Kuanzishwa mtandao wa intaneti wa “Qur'ani na Hadith” mjini Lahore, Pakistan

9:57 - February 04, 2009
Habari ID: 1739889
Mtandao wa intaneti wa “Qur'ani na Hadith” umeanzishwa mjini Lahore, Pakistan kwa lugha ya Kiurdu kwa msaada wa Chuo Kikuu cha Kidini cha “Jamiatul Ashrafiya”.
Kwa mujibu wa Idara ya Utamaduni ya Iran mjini Lahore, Maulana Muhammad Ubaidullah Rais wa Chuo Kikuu cha Kidini cha “Jamiatul Ashrafiya” ameshiriki katika sherehe za uzinduzi wa ukurasa huo wa intaneti wa “Qur'ani na Hadith” wa mji wa Lahore na kutoa maelezo kuhusu mtandao huo kwa hadhirina.
Aidha katika hafla hiyo, Maulana Hafidh Fadhlulrahman, afisa anayeshughulikia masomo katika Chuo Kikuu cha Kidini cha na wanazuoni kadhaa wa nchi hiyo walihudhuria sherehe za uzinduzi wa ukurasa huo wa intaneti. 357612

captcha