IQNA

Wanasesere wa kufundisha Qur'ani kwa ajili ya watoto wa Kiislamu kuanza kuuzwa nchini Uingereza

9:55 - February 09, 2009
Habari ID: 1742108
Wanasesera wa Kiislamu wataanza kuuzwa katika maduka makubwa ya Asda ya Uingereza mwezi ujao kwa ajili ya kuwafundisha watoto wa Kiislamu istilahi na maana ya sura za Qur'ani Tukufu.
Gazeti la Telegraph limeandika kuwa lengo la kuzalisha wanasesere hao ni kuwafunza watoto wa wahajiri wa Kiislamu nchini Uingereza istilahi za Qur'ani kupitia michezo na kwa njia za kuburudisha.
Mkuu wa shirika linalozalisha wanasesere hao Farzan Rahman amesema: "Nilipokuwa mtoto mdogo nilikuwa nikienda msikitini kila siku kwa ajili ya kujifunza na kuhifadhi Qur'ani, suala ambalo halikuwa na mvuto mkubwa kwangu. Uzalishaji wa wanasesere hawa utawawezesha watoto kujifunza Qur'ani kwa njia za kuburudisha na kuvutia."
Wanasesere hao wanazungumza na kusoma istilahi, ibara na sura za Qur'ani na tarjuma yake ya lugha ya Kiingereza kwa kubonyezwa miguu. 361127
captcha