Kituo cha habari cha Akhbarul Alam kimeandika kuwa Mahakama ya Rufaa ya Afghanistan imetoa hukumu hiyo kwa sababu ya upotoshaji uliomo katika tarjumi hiyo ya Qur'ani kwa lugha ya Kiafghani na madai ya utume yaliyotolewa na watarjumi wake.
Waafghani hao wawili waliojulikana kwa majina ya Amad Ghauth Zalmai ambaye ni mwandishi habari, na Sheikh Qari Mushtaq Ahmad, mwaka 2007 walichapisha tarjumi ya Qur'ani kwa lugha ya Kiafghani bila ya kufanya mlinganisho na matini yake ya asili kisha wakaigawa bure miongoni mwa wananchi.
Tarjumi hiyo ya Qur'ani ilikosolewa mno na wanafikra wa Kiislamu wa Afghanistan ambao waliwataja watarjumi hao kuwa ni makafiri na wakataka wahukumiwe kifo. 365175