IQNA

Nakala za Qur'ani zilizoandikwa kwa maandishi ya mkono zahifadhiwa Ethiopia

11:22 - April 05, 2009
Habari ID: 1760385
Majmui ya nakala za Qur'ani Tukufu zilizoandikwa kwa hati za mkono za Kituo cha Uhakiki cha Chuo Kikuu cha Addis Ababa zimetayarishwa na kuhifadhiwa kwa mujibu wa viwango vya kimataifa.
Kazi hiyo imefanyika kwa ufadhili wa Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Ethiopia.
Makumi ya nakala za Qur'ani zilizoandikwa kwa hati za mkono zilipewa utambulisho na alama maalumu katika shughuli iliyodumu kwa kipindi cha mwezi mmoja na nusu.
Mkataba wa kutimiza kazi hiyo ulitiwa saini mwezi Januari mwaka huu kati ya Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran mjini Addis Ababa na Mwenyekiti wa Kituo cha Uhakiki cha Chuo Kikuu cha Addis Ababa. 382436

captcha