IQNA

Mkutano wa Wakurugenzi wa Jumuiya za Qur'an wafanyika Uturuki

15:35 - April 06, 2009
Habari ID: 1761107
Mkutano wa Wakurugenzi wa jumuiya za Qur'ani Tukufu za eneo la Ulaya Mashariki na Uturuki wamekutana katika mji mkuu wa Uturuki Istanul. Mkutano huo unasimamiwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC na Jumuiya ya Kimataifa ya Kuhifadhi Qur'ani Tukufu.
Mkutano huo unahudhuriwa na wataalamu kutoka nchi za Uturuki, Bosnia Herzegovina, Kosovo, Albania, Ukraine, Bulgaria, Macedonia, Montenegro na Hungary.
Malengo ya mkutano huo yametajwa kuwa ni pamoja na kuweka mikakati ya kustawisha uhusiano kati ya taasisi na jumuiya zinazoshughulikia masala ya Qur'ani katika nchi hizo, kubadilishana uzoefu katika mafunzo na taaluma ya Qur'ani, kubuni mbinu mpya za kufunza kitabu hicho na kuandika mitaala ya masomo ya Qur'ani kwa ajili ya shule za nchi zilizotajwa. 382992

captcha