IQNA

Tarjumi mpya ya Qur'ani kwa wasomaji wa lugha ya Kiswahili yatolewa

17:00 - April 07, 2009
Habari ID: 1761678
Tarjumi kamili ya Qur'ani Tukufu imeanza kusambazwa na Kitengo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Tanzania. Tarjumi hiyo imeandikwa na Sheikh Ali Juma Mayunga na kuhaririwa na Taasisi ya Ansariyan mjini Qum nchini Iran.
Nakala 2500 za tarjumi hiyo ya Qur'ani zimekabidhiwa kwa Sheikh Ali Juma Mayunga kwa ajili ya kusambazwa katika maeneo mbalimbali ya Tanzania.
Tarjumi hiyo imeambatanishwa na tafsiri ya "Khulasatu Tafsiri" iliyoandikwa na Sheikh Mahmoud Tehrani. 383720

captcha