Msikiti na Chuo cha Sayansi ya Qur’ani cha al Saleh vilifunguliwa jana katika mji mkuu wa Yemen Sanaa. Sherehe za ufunguzi wa msikiti na chuo hicho zimehudhuriwa na Mshauri wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambaye pia ni Mkuu wa Jumuiya ya Utamaduni na Mawasiliano ya Kiislamu Mahdi Mustafawi na shakhsia wengine kadhaa wa ulimwengu wa Kiislamu.
Shirika rasmi la habari la Yemen SABA limeripoti kuwa sherehe za uzinduzi wa kituo hicho zilihudhuriwa pia na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Nchi za Kiislamu OIC Ekmeleddin Ihsanoglu, Rais wa Yemen Abdullah Saleh, Sheikh wa Chuo Kikuu cha al Azhar Muhammad Tantawi, Mufti wa Misri Ali Juma, Waziri wa Waqfu wa Saudi Arabia Saleh bin Abdulaziz Al Sheikh na wasomi kadhaa wa ulimwengu wa Kiislamu.
Naibu Waziri wa Waqfu wa Yemen amesema, hotuba kadhaa zilitolewa katika ufunguzi wa msikiti na chuo hicho cha sayansi ya Qur’ani ambazo zilijadili mchango na ujumbe wa dini, historia na utamaduni wa misikiti katika maisha ya Waislamu. 323467