IQNA

Mwanamke mwenye umri wa miaka 74 wa Kipalestina ahifadhi Qur'ani nzima

14:56 - September 05, 2010
Habari ID: 1988029
Bibi Rifqa Ahmad Abu Marsa amefanikiwa kuhifadhi Qur'ani nzima akiwa na umri wa miaka 74 kazi ambayo imewashinda vijana wengi.
Bibi Rifqa Ahmad anasema kwamba hakudhani kuwa anaweza kuhifadhi Qur'ani nzima katika umri kama wake lakini amefanikiwa kufanya kazi hiyo kwa irada na uwezo wake Mwenyezi Mungu.
Amesema: "Nilianza kuhifadhi Qur'ani miaka mine iliyopita wakati wa kuasisiwa msikiti wa Darul Qur'ani jinari na nyumbani kwangu na nikaanza kushiriki kwenye vikao vya tajwidi." Anaendelea kusimulia kwamba alishindwa kuendelea kushiriki kwenye masomo ya Qur'ani msikiti hapo kutokana na udhaifu wa kuona na hapo ndipo alipochukua uamuzi wa kuhifadhi Qur'ani ili athibitishe kwamba anaweza kuhifadhi kitabu hicho licha ya tatizo la macho. 648444

captcha