IQNA

ISESCO inafadhili shughuli za Qur'ani kote duniani hasa Afrika

12:40 - November 21, 2019
Habari ID: 3472225
TEHRAN (IQNA) - Shirika la Kiislamu la Elimu Sayansi na Utamaduni (ISESCO) limetangaza kuwa linaendesha shughuli 50 za Qur'ani Tukufu kila mwaka.

Akizungumza na IQNA, Gholamreza Karimu Mkuu wa Tume ya Kitaifa ya ISESCO nchini Iran amesema shughuli hizo zinajumuisha kuwafunza waalimu wa Qur'ani, kuinia kiwango cha taasisi za Qur'ani katika nchi mbali mbali hasa barani Afrika sambamba na kustawisah ufundishaji lugha ya Kiarabu ambayo ni lugha ya Qur'ani.

ISESCO ni taasisi ya Jumuiya ya Ushirikiano wa Nchi za Kiislamu OIC na ilianzishwa Mei mwaka 1979. ISESCO ndio taasisi kubwa zaidi ya Kiislamu katika uga wa kimataifa inayoshughulikia masuala ya elimu, sayansi na utamaduni.

3858281

captcha