IQNA

Misikiti Kuwait yatekeleza tena kanuni za kukabiliana na COVID-19

20:54 - January 07, 2022
Habari ID: 3474778
TEHRAN (IQNA)-Misikiti nchini Kuwait imeanza kutekeleza kanuni za kukabiliana na ugonjwa wa COVID-19 baada ya maambukizi kuongezeka nchini humo.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kuwait,KUNA, waumini wanaoingia misikitini sasa wanatakiwa kutokaribiana, wavae barakao na kila moja abebe mkeka binafsi wa kusali.

Aidha ni sharti kubakia wazi madirisha na milango wakati wote wa  sala na hotuba.

Aidha katika vikao vya kusajili ndoa au nikah ni watu sita tu wataruhusiwa kushiriki kuanzia Januari 9.

Halikadhalika serikali imepiga marufuku mijumuiko yote katika maeneo ya umma kuanzia Januari 9 hadi Februari 28.

Siku ya Jumatano Kuwait ilisajili kesi 2,413 mpya za COVID-19 na kwa msingi huo hadi sasa watu 425, 455 wameambukizwa nchini humo huku waliofariki kutokana na ugonjwa huo wakiwa ni 2,469.

4026888

Kishikizo: kuwait misikiti covid 19
captcha