Nakala za kitabu kitukufu cha Qur'ani zilizotarjumiwa kwa lugha za Kifaransa, Kihispania na Kitamazight (lugha ya Mabarbari wa kaskazini mwa Afrika) zimesambazwa katika misikiti, vituo vya kuhifadhisha Qur'ani ma jumuiya za masuala ya kheri na utamaduni za Algeria.
Nakala hizo za tarjumi ya Qur'ani zimetolewa zawadi na Kituo cha Kuchapisha Qur'ani cha Madina. Kituo hicho pia kimetoa maelfu ya nakala za Qur'ani tukufu kwa ajili ya wananchi wa Algeria kwa mnasaba wa kukaribia mwezi mtukufu wa Ramadhani.
Katika upande mwingine Kituo cha Kuchapisha Qur'ani cha Madina kimechapisha Qur'ami kwa hati za Braille makhsusi kwa wasioona ambazo zitaanza kugawanywa bure kwa watu wa tabaka hilo katika mwezi wa Ramadhani. 627909