IQNA

Ratiba maalumu ya Jumuiya ya Kiislamu ya Ghadir ya Ufaransa katika mwezi wa Ramadhani

12:02 - August 18, 2010
Habari ID: 1976132
Jumuiya ya Kiislamu ya Ghadir ya nchini Ufaransa inatekeleza ratiba maalumu kwa ajili ya Waislamu wa nchi hiyo katika mwezi huu mtukufu wa Ramadhani.
Kwa mujibu wa tovuti ya jumuiya hiyo ya Kiislamu, dua ya Iftitaah imekuwa ikisomwa kila usiku kuanzia saa mbili, mara tu baada ya kuswaliwa swala za Maghrib na Ishaa. Baada ya kufuturu pia kunakuwa na kikao cha kujibu maswali mbalimbali yanayoulizwa na washiriki. Wanazuoni wawili kutoka Lebanon ndio wanaojibu maswali hayo.
Vilevile Kituo cha Kiislamu cha Zeinab katika eneo la Courneuve kimekuwa kikitekeleza ratiba maalumu za mwezi wa Ramadhani. Ratiba hizo ni pamoja na kusoma Qur'ani, dua ya Iftitaah na dua ya Kumeil katika usiku wa kuamkia Ijumaa.
Ratiba nyingine ni kutoa futari na kuandaa darasa maalumu za kidini katika mwezi huu. 635699
captcha