IQNA

Viongozi wa Florida wakataa kutoa kibali cha siku ya kuchomwa moto Qur'ani

15:17 - August 21, 2010
Habari ID: 1977944
Viongozi wa serikali katika jimbo la Florida nchini Marekani wamekataa ombi la makasisi wa Kikristo wanaopiga vita Uislamu la kutoa kibali cha kuchomwa moto Qur'ani kadamnasi na mbele ya halaiki ya watu.
Kanisa na mji wa Jacksonville katika jimbo la Florida ambalo limeitangaza siku ya tarehe 11 Septemba kuwa ni siku ya kuchomwa moto Qur'ani, limewaandikia barua viongozi wa serikali ya jimbo hilo likiwataka waruhusu kitendo hicho cha kuchomwa moto hadharani kitabu cha Mwenyezi Mungu. Ombi hilo limepingwa vikali na viongozi hao.
Viongozi wa jimbo la Florida pia wamesema kuwa iwapo Qur’ani itachomwa moto hadharani kanisa la Jacksonville litalazimishwa kulipa faini na viongozi wake watafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.
Jumuiya na makundi ya Kiislamu katika nchi mbalimbali za Kiislamu yametangaza upinzani wao mkali dhidi ya kitendo hicho cha kukivunjia heshima kitabu cha Mwenyezi Mungu na wamewataka viongozi wa kanisa hilo kujiepusha na kitendo hicho. 637892

captcha