Taarifa ya Ayatullah Nur Mufid iliyotolewa kwa mnasaba wa njama ya kutaka kuchoma moto Qur'ani tukufu ya Kasisi Terry Jones wa Marekani imesema kuwa njama hiyo itagonga mwamba na kwamba Marekani na Wazayuni wanaojificha nyuma ya pazia ndio watakaolaumiwa kwa taathira zake mbaya na maumivu yaliyosababishwa na jinai hiyo katika nyoyo za Waislamu na wanafikra huru kote duniani.
Taarifa ya mwanazuoni huyo mkubwa wa kidini imesisitiza kuwa Qur'ani ni njia ya nuru, uongofu wa mwanadamu na mwongozo wa waumini na wacha-Mungu.
Ayatullah Nur Mufid amesema mpango uliobuniwa na kasisi jahili wa Florida nchini Marekani wa kuchoma moto Qur'ani ni dharau kubwa kwa matukufu ya Kiislamu na dini zote za Mwenyezi Mungu na unapaswa kulaani vikali.
Vilevile amezitaka jumuiya zote za Kiislamu na umma mzima wa Kiislamu kote duniani kuungana katika kukabiliana na mirengo inayuhujumu matukufu ya Kiislamu. 652953