IQNA

Mashindano ya kitaifa ya Qur'ani maalumu kwa vijana wa Kuwait

23:01 - September 19, 2010
Habari ID: 1997035
Mashindano ya 16 ya kitaifa ya Qur'ani Tukufu maalumu kwa vijana wa Kuwait yamepangwa kuanza Jumamosi tarehe 25 Septemba na kuendelea hadi Alkhamisi tarehe 30 Septemba.
Kwa mujibu wa gazeti la Kuwait la Anbaa mashindano hayo ambayo yatafanyika katika makundi mawili ya wanaume na wanawake yameandaliwa na Idara Kuu ya Vijana na Masuala ya Michezo ya Kuwait kwa ushirikiano wa Idara ya Masuala ya Qur'ani Tukufu ya Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Kuwait.
Jassim Ya'qub naibu mkuu wa idara iliyotajwa ya vijana amesema kuhusu suala hilo kwamba, mashindano hayo yatachangia pakubwa katika kuwajenga vijana na shakhsia zao za baadaye kwa misingi ya thamani za Kiislamu na Qur'ani.
Amesema, pia yatasaidia katika kuhudumia Qur'ani na kueneza utamaduni wa Kiislamu katika jamii ya Kuwait. 657754
captcha