Mashindano hayo yanasimamiwa na Taasisi ya Mama Kigezo ya Kuwait kwa ushirikiano wa Wizara ya Wakfu ya Masuala ya Kiislamu ya nchi hiyo.
Farija al Ahmad Mwenyekiti wa Taasisi ya Mama Kigezo amesema kuwa wanawake wa Kuwait wana fursa ya kujiandikisha kwa ajili ya kushiriki kwenye mashindano hayo hadi kufikia tarehe Mosi Oktoba.
Amesema kuwa mashindano hayo yatafanyika katika nyanja mbalimbali za kuhifadhi Qur'ani na kwamba washindi watatunukiwa zawadi za kati ya dinari 500 hadi 100 za Kuwait.
Farija al Ahmad amesema miongoni mwa malengo ya mashindano hayo ni kuzidisha maarifa ya kidini na kiutamaduni ya wanawake na kuimarisha uhusiano wa wananchi na Qur'an na vilevile kulea kizazi kipya kwa mujibu wa mafundisho na thamani za Qur'ani. 659547