IQNA

Washindi wa mashindano ya Qur'ani kwa walemavu wa akili waenziwa Misri

14:14 - September 21, 2010
Habari ID: 1998644
Washindi wa mashindano ya Qur'ani Tukufu makhsusi kwa ajili ya walemavu wa akili walienziwa na kutuzwa Jumatatu ya jana katika mji mkuu wa Misri Cairo.
Sherehe za kuwatunza washindi hao zilihudhuriwa na Khalid al Jundi, mhubiri mashuhuri wa Kiislamu na mkuu wa kanali ya televisheni ya satalaiti ya Azhari. Mashindano hayo ya Qur'ani ya walemavu wa akili ni ya kwanza kufanyika katika ulimwengu wa Kiislamu
Khalid al Jundi amesema kuwa televisheni moja ya Misri ina mpango wa kuanzisha kampeni ya misaada kwa mahafidhi wa Qur'ani wenye ulemavu wa akili ambayo itawawezesha kuhifadhi Qur'ani nzima.
Amesema kuwa ratiba nyingine za mpango huo ni kuwalea walemavu wa akili, kuwatayarishia maisha bora na fursa ya kupata elimu na malezi.
Mashindano hayo ya kwanza ya kitaifa ya Qur'ani ya walemavu wa akili yalifanyika mwezi uliopita chini ya usimamizi wa Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Misri. 659558


captcha