IQNA

Ukurasa wa Qur'ani kongwe kuuzwa mjini London

14:58 - September 27, 2010
Habari ID: 2002495
Ukurasa wa nakala ya zamani ya Qur'ani Tukufu iliyoandikwa katika nusu ya kwanza ya karne ya kwanza Hijria katika kipindi cha utawala wa Imam Ali bin Abi Twalib (as) utauzwa tarehe 16 Oktoba mjini London.
Mtandao wa habari wa Leblover umeripoti kuwa nakala hiyo ya zamani ya Qur'ani Tukufu ina kurasa 22 na imeandikwa kwa hati za Hijazi. Ukurasa huo una urefu wa sentimita 33 na upana wa sentimita 23 na bei yake inakadiriwa kuwa karibu dola laki mbili na 37 elfu.
Kituo cha minada cha Christy cha London hakikuashiria ukurasa huo wa Qur'ani ya zamani umepatikana wapi na unamilikiwa na nani.
Utafiti na chunguzi za kielimu zinaonyesha kuwa nakala zilizoandikwa katika zama za awali za Uislamu ziliandikwa kwa hati za Hijazi na bila kuwa na irabu. Herufi za nakala hizo pia hazikuwa na nukta juu au chini yake. 663640

captcha