IQNA

Wasomaji Qur'ani wa Karbalaa wakitembela Kituo cha Qur'ani cha Hadharat Ruqiyya (as) mjini Qum

11:47 - October 02, 2010
Habari ID: 2005214
Ujumbe wa wasomaji Qur'ani na wahudumu wa Haram ya Imam Hussein na Hadharat Abbas (as) umekitembelea Kituo cha Qur'ani cha Hadharat Ruqiyya (as) katika mji mtakatifu wa Qum.
Kwa mujibu wa tovuti ya Ruqayah.net, ujumbe huo ambao pia umemjumuisha Mustafa as-Swarraf, msomaji wa kimataifa wa Qur'ani, umekutana na kubadilishana mawazo na wakuu wa kituo hicho kuhusiana na njia za kubadilishana uzoefu kuhusiana na shughuli na ratiba za Qur'ani.
Katika mazungumzo hayo, wakuu wa kituo hicho cha Qur'ani waliwapa wageni wao zawadi ya vitabu, majarida na cd kadhaa za shughuli za kituo hicho.
Ujumbe huo wa pia umekutana na kundi la wasomaji kasida la al-Ghadir la mjini Qum na kubadilishana nalo uzoefu wa kisanaa katika uwanja wa masuala ya kidini. 666515
captcha