Kwa mujibu wa gazeti la Saudi Arabia la Iqtiswadiyyah, washiriki 87 wanashiriki katika mashindano hayo kama wahifadhi wa Qur'ani na wengine 38 katika kuhifadhi hadithi za Mtume (saw).
Washiriki wanatoka katika nchi 16 za Asia na eneo la Pacific.
Kuwashajiisha vijana wa Asia wahifadhi na kusoma Qur'ani Tukufu pamoja na kuhifadhi hadithi za Bwana Mtume (saw) na vilevile kuimarisha mfungamano wa vijana hao na Kitabu cha Mwenyezi Mungu ni baadhi ya malengo ya kufanyika mashindano hayo.
Sherehe za kushukuriwa na kuzawadiwa washindi wa mashindano hayo zitafanyika kesho Jumatatu ambapo rais wa Indonesia anatazamiwa kushiriki. 667421