Kwa mujibu wa tovuti ya kituo hicho, hafla ya kutolewa zawadi hizo itaanza mara tu baada ya kumalizika swala ya adhuhuri katika kituo hicho.
Mashindano hayo yaliyofanyika katika mwezi mtukufu wa Ramadhani na yaliyodhaminiwa na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu ya Saudi Arabia, yalifanyika katika hatua kadhaa za kuhifadhi juzuu moja, tano, kumi, ishirini na thelathini za Qur'ani Tukufu.
Lengo la kufanyika mashindano hayo lilitajwa kuwa ni kuwashajiisha Waislamu na hasa vijana wahifadhi Qur'ani na kujishughulisha na masuala ya Kiislamu na Qur'ani maishani. 679937