Stephan Wayld amesema katika kikao kilichotayarishwa na Kitengo cha Utafiti wa Mashariki ya Kati cha Chuo Kikuu cha Harvard kwamba kitabu kitakatifu cha Uislamu hakiwezi kutartumiwa kikamilifu na inavyotakikana kwa lugha nyingine na kinapotarjumiwa muujiza wa fasihi yake hutoweka.
Stephan Wayld ameongeza kuwa swali gumu katika kadhia hii ni jinsi ya kuweza kutarjumu Qur'ani Tukufu na wakati huo huo kulinda maana na ubora wa kifasihi wa kitabu hicho.
Mhadhiri huyo Mmarekani wa Chuo Kikuu cha Bonn amesisitiza juu ya kutarjumiwa Qur'ani Tukufu na wakati huo huo amekiri kwamba ni muhali kuweza kutarjumu kikamilifu maana ya kitabu hicho kwa lugha nyingine. 684654