IQNA

Nakala yenye umri wa miaka 1000 ya Qur’ani yagunduliwa China

14:02 - December 22, 2010
Habari ID: 2051750
Nakala ya Qur’ani yenye umri wa miaka elfu moja ilioandikwa kwa hati za mkono imegunduliwa hivi karibuni katika jimbo la Gansu huko kaskazini magharibi mwa China.
Nuskha hiyo ya Qur'an ambayo inaaminika kuwa ya kale zaidi nchini China iliandikwa kwa mkono katika karne ya 8 au 9 Miladia.
Kwa mujibu wa gazeti la People's Daily la China, wataalamu wanasema Qur'ani hiyo iliingizwa China kutoka Asia ya Kati.
Kutokana na muundo wa jaladi lake, nakshi, muundo wa kaligrafia na karatasi, Qur'ani hiyo inahesabiwa kuwa moja ya nuskha za kale zaidi za Qur'ani Tukufu duniani.
716356
captcha