IQNA

Kasisi aliyevunjia heshima Qur'ani kuitisha siku ya kimataifa ya kuihukumu Qur'ani

17:00 - January 12, 2011
Habari ID: 2063767
Kasisi aliyeivunjia heshima Qur'ani wa Marekani Terry Jones amechukua uamuzi wa kuitisha siku ya kimataifa ya kuihukumu Qur'ani.
Mtandao wa "MyFoxOrlando" umeripoti kuwa Kasisi Terry Jones wa kanisa na Gainesville katika jimbo la Florida ambaye mwaka jana alitishia kuchoma kitabu kitakatifu cha Qur'ani na kuzusha wimbi kubwa la malalamiko duniani kote, sasa amechukua hatua nyingine na kuamua kuitisha siku ya kimataifa ya kuihukumu Qur'ani!
Amesema kesho Jumatano tarehe 13 Januari atafanya mkutano na waandishi habari katika mji wa Gainesville na kutoa maelezo zaidi kuhusu mpango wake ambao amepanga kuutekeleza katika siku za kuanzia tarehe 1 hadi 30 Machi mwaka huu.
Kasisi Jones amesema kwa mujibu wa mpango huo Waislamu wanapaswa kuthibitisha kwamba Qur'ani ni kitabu kinachohubiri amani! 729169
captcha