Mashindano hayo ambayo yalidhaminiwa na Shirika la Huduma za Kibinadamu la As-Sheikh Thani bin Abdallah la Qatar yalifanyika kwa ushirikiano wa Baraza Kuu la Kiislamu la Mali na Taasisi ya Masuala ya Kheri ya Kiislamu ya nchi hiyo kwa jina la al-Farouq pamoja na msaada wa Waziri Mkuu wa Mali.
Duru ya kwanza ya mashindano hayo imewashirikisha washindani 57 katika makundi mawili ya wanawake na wanaume kutoka mikoa yote minane ya nchi hiyo ya Kiafrika.
Sherehe ya kuhitimisha mashindano hayo imefanyika katika ukumbi mkuu wa Kituo cha Mikutano ya Kimataifa cha Mali katika mji wa Bamako ambapo washindi wametunukiwa zawadi nono na za kuvutia. 741389