IQNA

Qari wa Kisuni Iran atembelewa na wajumbe wa Baraza Kuu la Qur'ani

13:52 - March 13, 2011
Habari ID: 2094543
Qari wa ngazi za juu wa Kisuni Abdul Rauf Changi Zehi katika mkoa wa Sistan na Baluchistan nchini Iran ametembelewa na ujumba wa Baraza Kuu la Qur'ani nchini.
Wajumbe wa Baraza Kuu la Qur'ani wamepokelewa na Abdul Rauf Changi Zehi ambaye pia ni Imamu wa Msikiti wa Othmaniya na mkurugenzi wa Chuo cha Kidini cha Faruqiah.
Kikao hicho kilichoanza na kisomo cha Qur'ani Tukufu kilikuwa fursa nzuri kwa pande mbili kujadili masuala ya Qur'ani katika mazingira ya kirafiki.
Safari hiyo ni katika fremu ya safari za wajumbe wa Baraza Kuu la Qur'ani la Iran katika maeneo mbalimbali ya nchi kwa lengo la kutafuta watu wenye vipawa vya Qur'ani, kukagua vituo cha Qur'ani na kuwaenzi wale wanaohudumia kitabu hicho kitakatifu hapa nchini.
761807
captcha