IQNA

Kongamano la Kimataifa la wakuu wa taasisi za Qur'ani kufanyika Sudan

17:53 - April 03, 2011
Habari ID: 2099907
Kongamano la kimataifa la mafunzo kwa wakuu wa taasisi za Qur'ani limepangwa kufanyika hapo kesho Jumatatu tarehe 4 hadi Jumatano tarehe 6 Aprili huko Khartoum , mji mkuu wa Sudan.
Kongamano hilo limeandaliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ISESCO kwa ushirikiano wa Jumuiya ya Kimataifa ya Kiislamu na vilevile Kamati ya Kitaifa ya Elimu, Utamaduni na Sayansi ya Sudan. Lengo la kufanyika kongamano hilo limetajwa kuwa ni kunyanyua kiwango cha masomo katika taasisi za Qur'ani, kutathmini shughuli za taasisi hizo na kutumiwa suhula za kisasa ikiwemo intaneti na kanali za satalaiti katika kuboresha masomo ya taasisi hizo. 767833
captcha