Imad Zahir Hafez mkuu wa mpango wa Tazim-ul-Qur'an amesema lengo lake ni kubainisha nafasi ya juu ya Qur'ani Tukufu, kuelezea miujiza ya kitabu hicho na kuwafahamisha Waislamu majukumu yao kuhusu Qur'ani.
"Kuwaelimusha watoto kuhusu nafasi ya Qur'ani na kuwahimiza kuimarisha uhusiano na kitabu hicho kitukufu, kuwaonya Waislamu kuhusu hatari za kuiacha Qur'ani na kukilinda kitabu hiki kitukufu kutokana na hujhuma za maadui ni kati ya malengo mengine ya mpango huu", amesema.
Ameelezea matumaini yake kuwa mpango wa Tazim-ul-Quran utakuwa mfano wa kuigwa katika ustawishaji wa mafundisho na thamani za Qur'ani Tukufu.
788426