IQNA

Nakala zaidi ya 5000 za Qur'ani zatolewa zawadi kwa nchi za Kiafrika

13:38 - May 15, 2011
Habari ID: 2122421
Jumuiya ya Risarat ya Misri imetoa zawadi ya nakala 5275 za Qur'ani Tukufuu kwa nchi za Kiafrika za Niger, Ivory Coast na Afrika Kusini.
Nakala hizo za Qur'ani zimetolewa na watetezi wa mazingira wa Jumuiya ya Masuala ya Kheri ya Risalat ya Misri.
Msemaji wa Jumuiya ya Masuala ya Kheri ya Risalat Marwa Abdul Maqsud amesema kuwa jumuiya hiyo imetuma Qur'ani hizo baada ya kugundua kwamba Waislamu wa nchi hizo za Afrika Kusini, Ivory Coast na Niger wanakabiliwa na uhaba wa nakala za Qur'ani Tukufu.
Jumuiya ya masuala ya kheri ya Risalat ya Misri ni miongoni mwa taasisi kubwa zaidi zenye matawi katika maeneo mbalimbali ya nchi hiyo na hujishughulisha zaidi na kutoa misaada kwa wahitaji, mayatima na watu wenye maradhi makhsusi. 791829

captcha