IQNA

Karatasi za shahsi zinazovunjia heshima Uislamu zapigwa marufuku

20:41 - May 31, 2011
Habari ID: 2131780
Maduka makubwa ya Carrefour ya Ufaransa na Ubelgiji yamesimamisha uuzaji wa karatasi za shashi zinazovunjia heshima matukufu ya Kiislamu katika maduka hayo.
Hatua hiyo imechukuliwa baada ya malalamiko makali ya Waislamu wa Ubelgiji.
Kituo cha habari cha 7sur7 kimeripoti kuwa maduka makubwa ya Carrefour yameamua kusimamisha uuzaji wa karatasi hizo za shashi zenye nakshi ya jina tukufu la Mtume Muhammad (saw) na jila la Mwenyezi Mungu la Allah baada ya Waislamu wa Ubelgiji kuwasilisha malalamiko makali dhidi ya kitendo hicho.
Waislamu wa Ubelgiji waliripoti suala hilo kwa maimami wa misikiti na baadaye jumuiya za Kiislamu zikawasilisha mashtaka dhidi ya kampuni iliyotengeneza makaratasi hayo ya kujifutia uchafu. 801471

captcha