IQNA

Warsha za kiraa ya Qur'ani kuandaliwa katika vyuo vikuu vya tiba Iran

16:55 - June 20, 2011
Habari ID: 2141338
Ili kuinua kiwango cha wasomaji Qur'ani, warsha maalumu zimepangwa kufanyika katika vyuo vikuu vya tiba katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Wizara ya Afya ya Iran inayosimamia vyuo vikuu vya tiba nchini imesema warsha hizo zitaendeshwa na makari mashuhuri.
Watakaoshiriki katika warsha hizo ni wahadhiri, wanachuo na wafanyakazi wa vyuo vikuu vya tiba.
Wataalamu wanatazamiwa kutatua matatizo ya kiraa ya watakaohudhuria warsha hizo.
Warsha ya kwanza ya kustawisha kiwango cha kiraa itafanyika katika Chuo Kikuu cha Sabzevar cha Sayansi za Tiba.
811252
captcha