Akibainisha suala hilo, Ra'd Adnan an-Nasiri mkuu wa kituo hicho cha Qur'ani amesema kuwa vikao hivyo vitafanyika kwa kuhudhuriwa na viongozi na maafisa wa kieneo wa mkoa huo. Amesema wasomaji Qur'ani wa mkoa huo waliovutiwa na kuiga kisomo cha Qur'ani cha Sheikh Shoaisha wamealikwa pia kushiriki kwenye vikao hivyo ili kuwakumbusha washiriki sauti na kisomo cha kuvutia cha marehemu huyo.
Sheikh Shoaisha ambaye pia alikuwa Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Makarii wa Misri aliaga dunia siku ya Alkhamisi iliyopita tarehe 24 Juni.